Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:61-66 Biblia Habari Njema (BHN)

61. “Umesikia matukano yao ee Mwenyezi-Mungu,na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.

62. Maneno na mawazo ya maadui zangu siku nzimani juu ya kuniangamiza mimi.

63. Wakati wote, wamekaa au wanakwenda,mimi ndiye wanayemzomea.

64. Uwalipize, ee Mwenyezi-Mungukadiri ya hayo matendo yao,kadiri ya mambo waliyotenda wenyewe.

65. Uipumbaze mioyo yao,na laana yako iwashukie.

66. Uwafuatie kwa hasira, uwaangamize,uwafanye watoweke ulimwenguni.”

Kusoma sura kamili Maombolezo 3