Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:48-61 Biblia Habari Njema (BHN)

48. Macho yangu yabubujika mito ya machozikwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.

49. “Machozi yatanitoka bila kikomo,

50. mpaka Mwenyezi-Mungu kutoka huko mbinguniaangalie chini na kuona.

51. Nalia na kujaa majonzi,kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.

52. “Nimewindwa kama ndegena hao wanichukiao bila sababu.

53. Walinitupa shimoni nikiwa haina juu yangu wakarundika mawe.

54. Maji yalianza kunifunika kichwa,nami nikafikiri, ‘Huu ni mwisho wangu.’

55. “Kutoka chini shimoninilikulilia ee Mwenyezi-Mungu.

56. Wewe umenisikia nikikulilia:‘Usiache kusikia kilio changu cha msaadabali unipatie nafuu.’

57. Nilipokuita ulinijia karibuukaniambia, ‘Usiogope!’

58. “Umenitetea katika kisa changu ee Mwenyezi-Mungu,umeyakomboa maisha yangu.

59. Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu,uniamulie kwa wema kisa changu.

60. Umeuona uovu wa maadui zangu,na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.

61. “Umesikia matukano yao ee Mwenyezi-Mungu,na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3