Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:41-59 Biblia Habari Njema (BHN)

41. Tumfungulie Mungu huko mbingunimioyo yetu na kumwomba:

42. “Sisi tulikukosea na kukuasinawe bado hujatusamehe.

43. “Umejizungushia hasira yako ukatufuatia,ukatuua bila huruma.

44. Umejizungushia wingu zito,sala yeyote isiweze kupenya humo.

45. Umetufanya kuwa takataka na uchafumiongoni mwa watu wa mataifa.

46. “Maadui zetu wote wanatuzomea.

47. Kitisho na hofu vimetuandama,tumepatwa na maafa na maangamizi.

48. Macho yangu yabubujika mito ya machozikwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.

49. “Machozi yatanitoka bila kikomo,

50. mpaka Mwenyezi-Mungu kutoka huko mbinguniaangalie chini na kuona.

51. Nalia na kujaa majonzi,kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.

52. “Nimewindwa kama ndegena hao wanichukiao bila sababu.

53. Walinitupa shimoni nikiwa haina juu yangu wakarundika mawe.

54. Maji yalianza kunifunika kichwa,nami nikafikiri, ‘Huu ni mwisho wangu.’

55. “Kutoka chini shimoninilikulilia ee Mwenyezi-Mungu.

56. Wewe umenisikia nikikulilia:‘Usiache kusikia kilio changu cha msaadabali unipatie nafuu.’

57. Nilipokuita ulinijia karibuukaniambia, ‘Usiogope!’

58. “Umenitetea katika kisa changu ee Mwenyezi-Mungu,umeyakomboa maisha yangu.

59. Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu,uniamulie kwa wema kisa changu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3