Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:4-13 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Amenichakaza ngozi na nyama,mifupa yangu ameivunja.

5. Amenizingira na kunizungushiauchungu na mateso.

6. Amenikalisha gizanikama watu waliokufa zamani.

7. Amenizungushia ukuta nisitoroke,amenifunga kwa minyororo mizito.

8. Ingawa naita na kulilia msaadaanaizuia sala yangu isimfikie.

9. Njia zangu ameziziba kwa mawe makubwaamevipotosha vichochoro vyangu.

10. Yeye ni kama dubu anayenivizia;ni kama simba aliyejificha.

11. Alinifukuza njiani mwangu,akanilemaza na kuniacha mkiwa.

12. Aliuvuta upinde wake,akanilenga mshale wake.

13. Alinichoma moyoni kwa mishale,kutoka katika podo lake.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3