Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:39-48 Biblia Habari Njema (BHN)

39. Kwa nini mtu anung'unike,ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?

40. Na tupime na kuchunguza mwenendo wetu,tupate kumrudia Mwenyezi-Mungu.

41. Tumfungulie Mungu huko mbingunimioyo yetu na kumwomba:

42. “Sisi tulikukosea na kukuasinawe bado hujatusamehe.

43. “Umejizungushia hasira yako ukatufuatia,ukatuua bila huruma.

44. Umejizungushia wingu zito,sala yeyote isiweze kupenya humo.

45. Umetufanya kuwa takataka na uchafumiongoni mwa watu wa mataifa.

46. “Maadui zetu wote wanatuzomea.

47. Kitisho na hofu vimetuandama,tumepatwa na maafa na maangamizi.

48. Macho yangu yabubujika mito ya machozikwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3