Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:26-37 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Ni vema mtu kungojea kwa saburiukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.

27. Ni vema mtu kujifunza uvumilivutangu wakati wa ujana wake.

28. Heri kukaa peke na kimya,mazito yanapompata kutoka kwa Mungu.

29. Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,huenda ikawa tumaini bado lipo.

30. Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,na kuwa tayari kupokea matusi yake.

31. Mwenyezi-Mungu hatatutupa milele.

32. Ingawa atufanya tuhuzunike,atakuwa na huruma tenakadiri ya wingi wa fadhili zake.

33. Yeye hapendelei kuwatesawala kuwahuzunisha wanadamu.

34. Wafungwa wote nchiniwanapodhulumiwa na kupondwa;

35. haki za binadamu zinapopotoshwambele yake Mungu Mkuu,

36. kesi ya mtu inapopotoshwa mahakamani,je, Mwenyezi-Mungu haoni hayo?

37. Nani awezaye kuamuru kitu kifanyikeMwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?

Kusoma sura kamili Maombolezo 3