Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:24-32 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yanguhivyo nitamwekea tumaini langu.

25. Mwenyezi-Mungu ni mwema kwa wanaomtegemea,ni mwema kwa wote wanaomtafuta.

26. Ni vema mtu kungojea kwa saburiukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.

27. Ni vema mtu kujifunza uvumilivutangu wakati wa ujana wake.

28. Heri kukaa peke na kimya,mazito yanapompata kutoka kwa Mungu.

29. Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,huenda ikawa tumaini bado lipo.

30. Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,na kuwa tayari kupokea matusi yake.

31. Mwenyezi-Mungu hatatutupa milele.

32. Ingawa atufanya tuhuzunike,atakuwa na huruma tenakadiri ya wingi wa fadhili zake.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3