Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Amenisagisha meno katika mawe,akanifanya nigaegae majivuni.

17. Moyo wangu haujui tena amani,kwangu furaha ni kitu kigeni.

18. Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”

19. Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangukwanipa uchungu kama wa nyongo.

20. Nayafikiria hayo daima,nayo roho yangu imejaa majonzi.

21. Lakini nakumbuka jambo hili moja,nami ninalo tumaini:

22. Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi,huruma zake hazina mwisho.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3