Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:15-30 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Amenijaza taabu,akanishibisha uchungu.

16. Amenisagisha meno katika mawe,akanifanya nigaegae majivuni.

17. Moyo wangu haujui tena amani,kwangu furaha ni kitu kigeni.

18. Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”

19. Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangukwanipa uchungu kama wa nyongo.

20. Nayafikiria hayo daima,nayo roho yangu imejaa majonzi.

21. Lakini nakumbuka jambo hili moja,nami ninalo tumaini:

22. Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi,huruma zake hazina mwisho.

23. Kila kunapokucha ni mpya kabisa,uaminifu wake ni mkuu mno.

24. Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yanguhivyo nitamwekea tumaini langu.

25. Mwenyezi-Mungu ni mwema kwa wanaomtegemea,ni mwema kwa wote wanaomtafuta.

26. Ni vema mtu kungojea kwa saburiukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.

27. Ni vema mtu kujifunza uvumilivutangu wakati wa ujana wake.

28. Heri kukaa peke na kimya,mazito yanapompata kutoka kwa Mungu.

29. Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,huenda ikawa tumaini bado lipo.

30. Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,na kuwa tayari kupokea matusi yake.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3