Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 1:17-22 Biblia Habari Njema (BHN)

17. “Nainyosha mikono yangulakini hakuna wa kunifariji.Mwenyezi-Mungu ametoa amri dhidi yangu mimi Yakobo,jirani zangu wawe maadui zangu.Naam, mimi Yerusalemu nimekuwa kinyaa kwao.

18. “Lakini Mwenyezi-Mungu amefanya sawakwa maana nimeliasi neno lake.Nisikilizeni enyi watu wote,yatazameni mateso yangu.Wasichana wangu na wavulana wangu,wamechukuliwa mateka.

19. “Niliwaita wapenzi wangu,lakini wao wakanihadaa.Makuhani na wazee wanguwamefia mjiniwakijitafutia chakula,ili wajirudishie nguvu zao.

20. “Ona, ee Mwenyezi-Mungu nilivyo taabuni.Roho yangu imechafuka,moyo wangu unasononekakwani nimekuasi vibaya.Huko nje kumejaa mauaji,ndani nako ni kama kifo tu.

21. “Sikiliza ninavyopiga kite;hakuna wa kunifariji.Maadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu:Wanafurahi kwamba umeniletea maafa.Uifanye ile siku uliyoahidi ifike,uwafanye nao wateseke kama mimi.

22. “Uwapatilize kwa ajili ya uovu wao wote.Uwatende kama ulivyonitenda mimikwa sababu ya makosa yangu yote.Nasononeka sana kwa maumivuna moyo wangu unazimia.”

Kusoma sura kamili Maombolezo 1