Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 40:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Ile madhabahu ya kuteketezea sadaka utaiweka mbele ya mlango wa hema takatifu la mkutano.

7. Birika la kutawadhia utaliweka katikati ya hema la mkutano na madhabahu na kulijaza maji.

8. Utazungushia ua na kutundika pazia penye lango lake.

9. “Kisha, utaliweka wakfu hema takatifu pamoja na vyombo vyake vyote kwa kuvipaka yale mafuta ya kupaka, nalo litakuwa takatifu.

10. Halafu, utaiweka wakfu madhabahu ya kuteketezea sadaka na vyombo vyake vyote kwa kuipaka mafuta, nayo itakuwa takatifu kabisa.

11. Birika la kutawadhia na tako lake pia utaliweka wakfu kwa namna hiyohiyo.

Kusoma sura kamili Kutoka 40