Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 40:5-15 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Madhabahu ya dhahabu ya kufukizia ubani utaiweka mbele ya sanduku la ushuhuda, kisha utatundika pazia kwenye mlango wa hema takatifu.

6. Ile madhabahu ya kuteketezea sadaka utaiweka mbele ya mlango wa hema takatifu la mkutano.

7. Birika la kutawadhia utaliweka katikati ya hema la mkutano na madhabahu na kulijaza maji.

8. Utazungushia ua na kutundika pazia penye lango lake.

9. “Kisha, utaliweka wakfu hema takatifu pamoja na vyombo vyake vyote kwa kuvipaka yale mafuta ya kupaka, nalo litakuwa takatifu.

10. Halafu, utaiweka wakfu madhabahu ya kuteketezea sadaka na vyombo vyake vyote kwa kuipaka mafuta, nayo itakuwa takatifu kabisa.

11. Birika la kutawadhia na tako lake pia utaliweka wakfu kwa namna hiyohiyo.

12. “Utamwita Aroni na wanawe waje mlangoni mwa hema la mkutano, kisha uwatawadhe.

13. Mvike Aroni yale mavazi matakatifu; utampaka mafuta na kumweka wakfu, ili aweze kunitumikia kama kuhani.

14. Waite wanawe na kuwavisha zile kanzu.

15. Kisha uwapake mafuta kama ulivyompaka baba yao, ili nao pia wanitumikie kama makuhani. Kupakwa mafuta huku kutawaingiza katika ukuhani wa kudumu katika vizazi vyao vyote.”

Kusoma sura kamili Kutoka 40