Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 39:33-36 Biblia Habari Njema (BHN)

33. Wakamletea Mose hema takatifu pamoja na vyombo vyake vyote, vikonyo vyake, mbao zake, pau zake, nguzo zake na vikalio vyake;

34. kifuniko cha ngozi za kondoo dume na mbuzi kilichotiwa rangi nyekundu, pazia la mahali patakatifu,

35. sanduku la agano, mipiko yake na kiti cha rehema;

36. meza na vyombo vyake vyote, mikate iliyowekwa mbele ya Mungu;

Kusoma sura kamili Kutoka 39