Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 39:24-28 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Kwenye upindo wa chini wa kanzu walifuma mapambo ya makomamanga ya rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa.

25. Kisha walitengeneza njuga za dhahabu, na kila baada ya komamanga walitia njuga kwenye upindo wa joho.

26. Hivyo, njuga na komamanga vilifuatana kuuzunguka upindo wa joho hilo, kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose.

27. Kisha wakawafumia Aroni na wanawe vizibao vya kitani safi,

28. kilemba cha kitani safi, kofia za kitani safi, suruali za kitani safi iliyosokotwa,

Kusoma sura kamili Kutoka 39