Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 39:11-16 Biblia Habari Njema (BHN)

11. safu ya pili ilikuwa ya zumaridi, na johari ya rangi ya samawati na almasi;

12. safu ya tatu ilikuwa ya yasintho, ya akiki nyekundu na amethisto;

13. na safu ya nne ilikuwa ya zabarajadi, ya shohamu na yaspi; yote yalimiminiwa vijalizo vya dhahabu.

14. Basi, palikuwa na mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Yalikuwa yamechorwa kama wachoravyo mhuri, kila moja limechorwa jina kuwakilisha makabila kumi na mawili.

15. Walikitengenezea kile kifuko cha kifuani mikufu ya dhahabu safi.

16. Walitengeneza vijalizo viwili vya dhahabu safi na pete mbili za dhahabu, na kuzitia pete hizo kwenye ncha mbili za juu za kifuko hicho.

Kusoma sura kamili Kutoka 39