Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 37:23-29 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Alikitengenezea taa saba, koleo na visahani vyake kwa dhahabu safi.

24. Alikitengeneza kinara hicho na vifaa vyake kwa kilo thelathini na tano za dhahabu.

25. Alitengeneza madhabahu ya kufukizia ubani kwa mbao za mjohoro. Madhabahu hiyo ilikuwa ya mraba, sentimita 45 kwa sentimita 45, na kimo chake sentimita 90. Pembe za madhabahu hiyo zilikuwa kitu kimoja na madhabahu yenyewe.

26. Yote aliipaka dhahabu safi: Upande wake wa juu, pande zake za ubavuni na pembe zake; pia aliitengenezea ukingo wa dhahabu.

27. Alitengeneza pete mbili za dhahabu chini ya ukingo kwenye pande mbili zinazokabiliana. Pete hizo zilitumika kushikilia mipiko ya kuibebea.

28. Alifanya mipiko miwili ya mjohoro na kuipaka dhahabu.

29. Alitengeneza mafuta matakatifu ya kupaka, na ubani safi wenye harufu nzuri uliochanganywa vizuri kama manukato.

Kusoma sura kamili Kutoka 37