Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 37:11-23 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Aliipaka dhahabu safi na kuitengenezea ukingo wa dhahabu.

12. Aliizungushia mviringo wa ubao wenye upana wa milimita 75, na kuifanyia ukingo wa dhahabu.

13. Aliitengenezea pete nne za dhahabu na kuzitia katika pembe zake nne mahali miguu ilipoishia.

14. Pete hizo za kushikilia ile mipiko ya kulibebea ziliwekwa karibu na ule mviringo wa ubao.

15. Alitengeneza mipiko miwili ya mjohoro ya kulibebea, akaipaka dhahabu.

16. Alitengeneza vyombo vya dhahabu safi vya kuweka juu ya meza: Sahani zake na visahani kwa ajili ya ubani, na bilauri zake na bakuli kwa ajili ya tambiko za kinywaji.

17. Alitengeneza pia kinara cha taa kwa dhahabu safi. Tako lake, na ufito wa hicho kinara ulikuwa kitu kimoja pamoja na vikombe vyake, matumba yake na maua yake.

18. Matawi sita yalitokeza kila upande wa ufito wake, matawi matatu upande mmoja na matawi matatu upande mwingine.

19. Katika kila tawi kulikuwa na vikombe vitatu mfano wa maua ya mlozi, kila kimoja na tumba lake na ua lake.

20. Na katika ufito kulikuwa na vikombe vinne mfano wa maua ya mlozi, pamoja na matumba yake na maua yake.

21. Mahali pale palipotokezea jozi tatu za matawi chini ya kila jozi kulikuwa na tumba moja.

22. Matumba hayo na matawi vilikuwa kitu kimoja na kinara hicho, na chote kilifuliwa kwa dhahabu safi.

23. Alikitengenezea taa saba, koleo na visahani vyake kwa dhahabu safi.

Kusoma sura kamili Kutoka 37