Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 37:11-17 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Aliipaka dhahabu safi na kuitengenezea ukingo wa dhahabu.

12. Aliizungushia mviringo wa ubao wenye upana wa milimita 75, na kuifanyia ukingo wa dhahabu.

13. Aliitengenezea pete nne za dhahabu na kuzitia katika pembe zake nne mahali miguu ilipoishia.

14. Pete hizo za kushikilia ile mipiko ya kulibebea ziliwekwa karibu na ule mviringo wa ubao.

15. Alitengeneza mipiko miwili ya mjohoro ya kulibebea, akaipaka dhahabu.

16. Alitengeneza vyombo vya dhahabu safi vya kuweka juu ya meza: Sahani zake na visahani kwa ajili ya ubani, na bilauri zake na bakuli kwa ajili ya tambiko za kinywaji.

17. Alitengeneza pia kinara cha taa kwa dhahabu safi. Tako lake, na ufito wa hicho kinara ulikuwa kitu kimoja pamoja na vikombe vyake, matumba yake na maua yake.

Kusoma sura kamili Kutoka 37