Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 35:30-35 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Mose aliwaambia Waisraeli; “Tazameni! Mwenyezi-Mungu amemteua Bezaleli, mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda.

31. Amemjaza roho yake, amempa ujuzi, akili, maarifa na ufundi,

32. abuni michoro ya sanaa na kufanya kazi za kufua dhahabu, fedha na shaba;

33. achonge mawe ya kupambia na mbao kwa ajili ya kazi nyingine zote za kifundi.

34. Pia amemwongoza yeye na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani wawafundishe wengine.

35. Amewapa ujuzi wa kufanya kila kazi ya ufundi au ifanywayo na watu wa sanaa au mafundi wa kutarizi kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kwa kutumia ufundi wowote wa msanii.

Kusoma sura kamili Kutoka 35