Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 35:24-28 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Kila mtu aliyeweza kutoa fedha au shaba aliileta kwa Mwenyezi-Mungu kama toleo lake. Tena mtu yeyote aliyekuwa na mbao za mjohoro alileta pia.

25. Wanawake wote waliokuwa na ujuzi wa kufuma walileta vitu walivyofuma kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa.

26. Na wanawake wote waliokuwa na ujuzi walisokota manyoya ya mbuzi.

27. Viongozi walileta vito vya rangi na mawe mengine kwa ajili ya kizibao na kifuko cha kifuani;

28. walileta pia viungo na mafuta kwa ajili ya taa, mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri.

Kusoma sura kamili Kutoka 35