Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 35:11-18 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Kutengeneza hema takatifu, kifuniko chake na pazia lake, kulabu zake, pau zake, vikalio vyake;

12. sanduku la agano pamoja na mipiko yake, kiti cha rehema, pazia la mahali patakatifu sana;

13. meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate iliyowekwa mbele ya Mwenyezi-Mungu;

14. vinara vya taa pamoja na vyombo vyake vyote, taa zake na mafuta yake;

15. madhabahu ya ubani na mipiko yake, mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri, pazia la mlango wa hema takatifu;

16. madhabahu ya sadaka za kuteketezwa pamoja na wavu wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, birika na tako lake;

17. vyandarua vya ua, nguzo zake na vikalio vyake, pazia la mlango wa ua;

18. vigingi vya hema takatifu na vya ua pamoja na kamba zake;

Kusoma sura kamili Kutoka 35