Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 35:10-15 Biblia Habari Njema (BHN)

10. “Kila mtu mwenye ujuzi wa kazi fulani miongoni mwenu atakuja kufanya vitu vyote alivyoamuru Mwenyezi-Mungu:

11. Kutengeneza hema takatifu, kifuniko chake na pazia lake, kulabu zake, pau zake, vikalio vyake;

12. sanduku la agano pamoja na mipiko yake, kiti cha rehema, pazia la mahali patakatifu sana;

13. meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate iliyowekwa mbele ya Mwenyezi-Mungu;

14. vinara vya taa pamoja na vyombo vyake vyote, taa zake na mafuta yake;

15. madhabahu ya ubani na mipiko yake, mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri, pazia la mlango wa hema takatifu;

Kusoma sura kamili Kutoka 35