Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 33:16-23 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Maana nitajuaje kuwa nimepata fadhili mbele zako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee miongoni mwa watu wote duniani.”

17. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kwa kuwa umepata fadhili mbele yangu, nami nakujua kwa jina lako, jambo hilihili ulilolisema nitalifanya.”

18. Mose akasema, “Nakusihi unioneshe utukufu wako.”

19. Mwenyezi-Mungu akamjibu, “Nitapita mbele yako na kukuonesha wema wangu wote nikilitangaza jina langu, ‘Mwenyezi-Mungu’. Mimi nitamrehemu yule ninayependa kumrehemu, na kumhurumia yule ninayependa kumhurumia.

20. Lakini hutaweza kuniona uso maana hakuna mwanadamu yeyote atakayeniona na kuishi.”

21. Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kuna mahali karibu nami ambapo utasimama juu ya mwamba;

22. na utukufu wangu utakapokuwa unapita, nitakutia katika pango mwambani na kukufunika kwa mkono wangu, mpaka nitakapokuwa nimepita.

23. Halafu nitauondoa mkono wangu nawe utaniona nyuma, lakini uso wangu hutauona.”

Kusoma sura kamili Kutoka 33