Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 30:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,

18. “Utatengeneza birika la shaba la kutawadhia lenye tako la shaba, uliweke katikati ya hema la mkutano na madhabahu, na kutia maji ndani yake.

19. Aroni na wanawe watatumia maji hayo kunawia mikono na miguu,

20. kabla ya kuingia kwenye hema la mkutano au kukaribia madhabahu ili kunitolea tambiko mimi Mwenyezi-Mungu, tambiko zitolewazo kwa moto; watafanya hivyo wasije wakafa.

Kusoma sura kamili Kutoka 30