Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 29:42-46 Biblia Habari Njema (BHN)

42. Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa daima, kizazi hata kizazi, mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu, mbele ya mlango wa hema la mkutano ambapo mimi nitakutana nanyi na kuongea nanyi.

43. Hapo ndipo nitakapokutana na Waisraeli na utukufu wangu utapafanya pawe patakatifu.

44. Hema la mkutano na madhabahu nitavifanya vitakatifu; vilevile Aroni na wanawe nitawaweka wakfu ili wanitumikie kama makuhani.

45. Nitaishi kati ya Waisraeli, nami nitakuwa Mungu wao.

46. Hapo ndipo watakapotambua kuwa mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, niliyewaleta kutoka nchi ya Misri, ili niishi kati yao. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.

Kusoma sura kamili Kutoka 29