Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 28:12-18 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Mawe hayo mawili yatawekwa juu ya kanda za kizibao kama kumbukumbu ya makabila kumi na mawili ya Israeli. Hivyo Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu kama ukumbusho.

13. Utayatengenezea vijalizo viwili vya dhahabu,

14. na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba. Utaifunga mikufu hiyo kwenye hivyo vijalizo.

15. “Utatengeneza kifuko cha kifuani cha kauli cha maamuzi; kitengenezwe kwa ustadi sawa kama kilivyotengenezwa kile kizibao: Kwa dhahabu, kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa.

16. Kifuko hicho ambacho kimekunjwa kitakuwa cha mraba, sentimita 22.

17. Kitapambwa kwa safu nne za mawe ya thamani: Safu ya kwanza itakuwa ya akiki, topazi na almasi nyekundu;

18. safu ya pili itakuwa ya zumaridi, johari ya rangi ya samawati na almasi;

Kusoma sura kamili Kutoka 28