Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 26:21-30 Biblia Habari Njema (BHN)

21. na vikalio vyake arubaini vya fedha, vikalio viwili chini ya kila ubao.

22. Kwa upande wa nyuma, ulio magharibi ya hema, utatengeneza mbao sita.

23. Utatengeneza pia mbao mbili kwa ajili ya pembe za hema upande wake wa nyuma.

24. Mbao hizo za pembeni ziachane chini lakini zishikamanishwe kwa juu kwenye pete ya kwanza. Mbao zote za pembeni zifanywe vivyo hivyo ili zifanye pembe mbili.

25. Hivyo kutakuwa na mbao nane pamoja na vikalio vyake kumi na sita vya fedha: Vikalio viwili chini ya kila mbao na vikalio viwili chini ya ubao mwingine.

26. “Utatengeneza pau za mjohoro; pau tano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa hema,

27. na pau tano kwa ajili ya upande wa pili wa hema, na pau tano kwa ajili ya mbao za upande wa nyuma wa hema, ulio magharibi.

28. Upau wa katikati uliofika nusu ya jengo la hema utapenya katikati toka mwisho huu hadi mwisho mwingine wa hema.

29. Mbao zote utazipaka dhahabu na kuzifanyia pete za dhahabu zitakazoshikilia hizo pau, ambazo pia utazipaka dhahabu.

30. Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

Kusoma sura kamili Kutoka 26