Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 25:14-22 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Mipiko hiyo utaipitisha katika pete zilizo pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibebea.

15. Mipiko hiyo itabaki daima katika pete; isitolewe wakati wowote.

16. Ndani ya sanduku hilo utaweka vibao viwili vya mawe vya ushuhuda.

17. “Kisha utatengeneza kwa dhahabu safi kiti cha rehema, urefu wake sentimita 110, na upana wake sentimita 66.

18. Utatengeneza pia mfano wa viumbe hai viwili kwa kufua dhahabu, uviweke kwenye miisho miwili ya kiti hicho;

19. kiumbe kimoja mwisho mmoja na kiumbe kingine mwisho mwingine. Viweke viumbe hivyo kwenye miisho ya kiti hicho, lakini viwe kitu kimoja na hicho kiti.

20. Viumbe hivyo vitaelekeana, mabawa yake yamekunjuka kukifunika kiti cha rehema; nyuso zake zitaelekea kiti hicho.

21. Ndani ya sanduku utaweka vibao viwili vya mawe na kukiweka kiti cha rehema juu yake.

22. Mimi nitakutana nawe hapo; na kutoka juu ya kiti hicho cha rehema katikati ya viumbe hao walioko juu ya sanduku la ushuhuda, nitazungumza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.

Kusoma sura kamili Kutoka 25