Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 25:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,

2. “Waambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo, nawe upokee kwa niaba yangu. Utapokea kutoka kwa mtu yeyote atakayetoa kwa moyo mkunjufu.

3. Utapokea matoleo yafuatayo: Dhahabu, fedha, shaba,

4. sufu ya buluu, ya zambarau na nyekundu, kitani safi iliyosokotwa manyoya ya mbuzi;

5. ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi, mbao za mjohoro,

Kusoma sura kamili Kutoka 25