Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 22:19-29 Biblia Habari Njema (BHN)

19. “Anayezini na mnyama lazima auawe.

20. “Anayemtolea tambiko mungu mwingine badala ya Mwenyezi-Mungu pekee, lazima aangamizwe kabisa.

21. “Msimdhulumu mgeni wala kumtesa, maana nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri.

22. Msimtese mjane au yatima.

23. Kama mkiwadhulumu hao nao wakanililia, hakika nitakisikiliza kilio chao,

24. na hasira yangu itawaka, nami nitawaueni kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu yatima.

25. “Ukimkopesha fedha mtu yeyote miongoni mwa watu wangu walio maskini, usiwe kwake kama mdai, wala usimtoze riba.

26. Ukilichukua vazi la mwenzako kuliweka rehani, lazima umrudishie kabla ya jua kutua,

27. kwa kuwa hiyo ndiyo nguo yake ya pekee; ndiyo atakayojifunika nayo. Au wadhani atalalia nini? Akinililia nitamsikiliza, maana mimi ni mwenye huruma.

28. “Usimtukane Mungu, wala kumlaani mkuu wa watu wako.

29. “Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mtanipa wazaliwa wenu wa kwanza wa kiume.

Kusoma sura kamili Kutoka 22