Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 22:17-26 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Baba wa huyo msichana akikataa katakata kumwoza binti yake, mtu huyo atalipa fedha ya mahari inayostahili msichana aliye bikira.

18. “Usimwache mwanamke mchawi aishi.

19. “Anayezini na mnyama lazima auawe.

20. “Anayemtolea tambiko mungu mwingine badala ya Mwenyezi-Mungu pekee, lazima aangamizwe kabisa.

21. “Msimdhulumu mgeni wala kumtesa, maana nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri.

22. Msimtese mjane au yatima.

23. Kama mkiwadhulumu hao nao wakanililia, hakika nitakisikiliza kilio chao,

24. na hasira yangu itawaka, nami nitawaueni kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu yatima.

25. “Ukimkopesha fedha mtu yeyote miongoni mwa watu wangu walio maskini, usiwe kwake kama mdai, wala usimtoze riba.

26. Ukilichukua vazi la mwenzako kuliweka rehani, lazima umrudishie kabla ya jua kutua,

Kusoma sura kamili Kutoka 22