Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 21:9-16 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Kama ataamua kumwoza kwa mwanawe, atamtendea mtumwa huyo kama binti yake.

10. Kama huyo bwana akioa mke mwingine, lazima aendelee kumtosheleza mkewe wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zake za ndoa.

11. Iwapo huyo bwana hatamtimizia haki hizo tatu, basi, mke ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote.

12. “Ampigaye mtu na kumwua, lazima auawe.

13. Lakini kama hakuwa amemvizia, bali ni kwa ajali, basi, huyo mwuaji ataweza kukimbilia usalama mahali nitakapowachagulieni.

14. Lakini mtu akimshambulia mwenzake makusudi na kumwua kwa ujeuri, hata kama atakimbilia kwenye madhabahu, mtamtoa huko madhabahuni pangu na kumwua.

15. “Ampigaye baba yake au mama yake lazima auawe.

16. “Amtekaye mtu nyara ili kumwuza au kumfanya mtumwa wake lazima auawe.

Kusoma sura kamili Kutoka 21