Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 20:18-21 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kuisikia sauti ya parapanda juu ya mlima uliokuwa unafuka moshi, wote waliogopa na kutetemeka. Wote walisimama mbali,

19. wakamwambia Mose, “Ongea nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza, lakini Mwenyezi-Mungu asiongee nasi, tusije tukafa.”

20. Mose akawaambia, “Msiogope, maana Mungu amekuja kuwajaribu ili mpate kumcha yeye daima na msitende dhambi.”

21. Watu wote walisimama mbali wakati Mose alipokaribia lile wingu zito alimokuwamo Mungu.

Kusoma sura kamili Kutoka 20