1. Mwenyezi-Mungu alizungumza maneno haya yote, akasema,
2. “Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, niliyekutoa nchini Misri, ambako ulikuwa mtumwa.
3. “Usiwe na miungu mingine ila mimi.
4. “Usijifanyie sanamu ya miungu wa uongo, au kinyago cha chochote kilicho mbinguni, katika nchi au majini chini ya dunia.