Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 2:22-25 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Zipora akamzalia mtoto wa kiume. Mose akasema, “Nimekimbilia katika nchi ya kigeni”, kwa hiyo akampa huyo mtoto jina Gershomu.

23. Baada ya muda mrefu, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli wakapiga kite na kulia kutokana na hali yao ya utumwa, na kilio chao kikamfikia Mungu juu.

24. Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, na Isaka na Yakobo.

25. Mungu aliwaangalia Waisraeli, akaona kuwa hali yao ni mbaya.

Kusoma sura kamili Kutoka 2