Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 18:15-19 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Mose akamjibu mkwewe, “Kwa sababu watu huja kwangu kuuliza matakwa ya Mungu.

16. Wakiwa na ugomvi wowote ule wao huja kwangu nami huamua kati ya mtu na mwenzake, na kuwafunza amri za Mungu na maamuzi yake.”

17. Basi, Yethro akamwambia Mose, “Unavyofanya si vizuri!

18. Utajidhuru mwenyewe na hawa watu kwa uchovu, kwani hii ni kazi ngumu usiyoweza kuifanya peke yako.

19. Sikiliza shauri langu kwako, na Mungu awe pamoja nawe. Wewe utawawakilisha watu mbele ya Mungu na kumletea Mungu matatizo yao.

Kusoma sura kamili Kutoka 18