Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 15:6-15 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu watukuka kwa nguvu;kwa mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu wawaponda adui.

7. Kwa wingi wa ukuu wako wawaangamiza wapinzani wako;wawapulizia ghadhabu yako nayo yawateketeza kama makapi.

8. Kwa pumzi ya pua yako maji yalirundikana,mawimbi yakasimama wima kama ukuta;vilindi katikati ya bahari vikagandamana.

9. Adui alijisemea, ‘Nitawafuata na kuwakamata;nitagawanya nyara mpaka hamu yangu iishe.Tutaufuta upanga wetu,tutawaangamiza kwa mkono wetu.’

10. Lakini wewe uliuvumisha upepo wako,nayo bahari ikawafunika.Walizama majini kama risasi.

11. “Ewe Mwenyezi-Mungu,ni nani kati ya miungu anayelingana nawe?Ni nani aliye kama wewe uliye mtakatifu mkuu,utishaye kwa matendo matukufu,unayetenda mambo ya ajabu?

12. Uliunyosha mkono wako wa kulia,nayo nchi ikawameza maadui zetu.

13. “Kwa fadhili zako kuu umewaongoza watu uliowakomboa,kwa nguvu yako umewaongoza kwenye makao yako matakatifu.

14. Watu wa mataifa wamesikia hayo wakatetemeka;wakazi wa Filistia wamekumbwa na kitisho.

15. Wakuu wa Edomu wamefadhaishwa;viongozi wa Moabu wamekumbwa na woga mkuu;wakazi wote wa Kanaani wamevunjika moyo.

Kusoma sura kamili Kutoka 15