15. Wakuu wa Edomu wamefadhaishwa;viongozi wa Moabu wamekumbwa na woga mkuu;wakazi wote wa Kanaani wamevunjika moyo.
16. Kitisho na hofu vimewavamia.Kwa sababu ya ukuu wa nguvu zako,wao wamenyamaza kimya kama jiwe,mpaka watu wako ee Mwenyezi-Mungu, wapite,naam, mpaka watu hao uliowakomboa wamewapita.
17. Wewe utawaleta watu wako na kuwapanda mlimani pako;pale ulipochagua ee Mwenyezi-Mungu pawe makao yako,mahali patakatifu ee Mwenyezi-Mungu ulipojenga kwa mikono yako.
18. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu,watawala milele na milele.”