Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 15:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Wakuu wa Edomu wamefadhaishwa;viongozi wa Moabu wamekumbwa na woga mkuu;wakazi wote wa Kanaani wamevunjika moyo.

16. Kitisho na hofu vimewavamia.Kwa sababu ya ukuu wa nguvu zako,wao wamenyamaza kimya kama jiwe,mpaka watu wako ee Mwenyezi-Mungu, wapite,naam, mpaka watu hao uliowakomboa wamewapita.

17. Wewe utawaleta watu wako na kuwapanda mlimani pako;pale ulipochagua ee Mwenyezi-Mungu pawe makao yako,mahali patakatifu ee Mwenyezi-Mungu ulipojenga kwa mikono yako.

18. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu,watawala milele na milele.”

Kusoma sura kamili Kutoka 15