Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 15:11-18 Biblia Habari Njema (BHN)

11. “Ewe Mwenyezi-Mungu,ni nani kati ya miungu anayelingana nawe?Ni nani aliye kama wewe uliye mtakatifu mkuu,utishaye kwa matendo matukufu,unayetenda mambo ya ajabu?

12. Uliunyosha mkono wako wa kulia,nayo nchi ikawameza maadui zetu.

13. “Kwa fadhili zako kuu umewaongoza watu uliowakomboa,kwa nguvu yako umewaongoza kwenye makao yako matakatifu.

14. Watu wa mataifa wamesikia hayo wakatetemeka;wakazi wa Filistia wamekumbwa na kitisho.

15. Wakuu wa Edomu wamefadhaishwa;viongozi wa Moabu wamekumbwa na woga mkuu;wakazi wote wa Kanaani wamevunjika moyo.

16. Kitisho na hofu vimewavamia.Kwa sababu ya ukuu wa nguvu zako,wao wamenyamaza kimya kama jiwe,mpaka watu wako ee Mwenyezi-Mungu, wapite,naam, mpaka watu hao uliowakomboa wamewapita.

17. Wewe utawaleta watu wako na kuwapanda mlimani pako;pale ulipochagua ee Mwenyezi-Mungu pawe makao yako,mahali patakatifu ee Mwenyezi-Mungu ulipojenga kwa mikono yako.

18. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu,watawala milele na milele.”

Kusoma sura kamili Kutoka 15