Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 15:1-11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hapo, Mose pamoja na Waisraeli wakamwimbia Mwenyezi-Mungu wimbo huu,“Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu kwani ameshinda kwa fahari,farasi na mpandafarasi wake amewatosa baharini.

2. Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu na uwezo,yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.Yeye ni Mungu wangu nami nitamsifu,ni Mungu wa baba yangu nami nitamtukuza.

3. Mwenyezi-Mungu ni shujaa vitani;Mwenyezi-Mungu ndilo jina lake.

4. “Magari na majeshi ya Farao ameyatumbukiza baharini,maofisa wake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.

5. Vilindi vya maji vimewafunika,wameporomoka baharini kama jiwe.

6. “Mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu watukuka kwa nguvu;kwa mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu wawaponda adui.

7. Kwa wingi wa ukuu wako wawaangamiza wapinzani wako;wawapulizia ghadhabu yako nayo yawateketeza kama makapi.

8. Kwa pumzi ya pua yako maji yalirundikana,mawimbi yakasimama wima kama ukuta;vilindi katikati ya bahari vikagandamana.

9. Adui alijisemea, ‘Nitawafuata na kuwakamata;nitagawanya nyara mpaka hamu yangu iishe.Tutaufuta upanga wetu,tutawaangamiza kwa mkono wetu.’

10. Lakini wewe uliuvumisha upepo wako,nayo bahari ikawafunika.Walizama majini kama risasi.

11. “Ewe Mwenyezi-Mungu,ni nani kati ya miungu anayelingana nawe?Ni nani aliye kama wewe uliye mtakatifu mkuu,utishaye kwa matendo matukufu,unayetenda mambo ya ajabu?

Kusoma sura kamili Kutoka 15