Agano la Kale

Agano Jipya

Kutoka 1:6-10 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Baadaye, Yosefu alifariki, hali kadhalika ndugu zake na kizazi kile chote.

7. Lakini wazawa wa Israeli waliongezeka sana, wakawa wengi na wenye nguvu mno, wakaenea kila mahali nchini Misri.

8. Basi, akatokea mfalme mwingine huko Misri ambaye hakumjua Yosefu.

9. Naye akawaambia watu wake, “Tazameni jinsi Waisraeli walivyo wengi na wenye nguvu kuliko sisi.

10. Ni lazima tutafute hila ya kuwapunguza na kuzuia wasiongezeke; la sivyo, kama vita vikitokea watajiunga na adui zetu na kuitoroka nchi.”

Kusoma sura kamili Kutoka 1