1. Haya ndiyo majina ya watoto wa kiume wa Israeli, ambao walikwenda Misri, kila mmoja na jamaa yake:
2. Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda,
3. Isakari, Zebuluni, Benyamini,
4. Dani, Naftali, Gadi na Asheri.
5. Wazawa wote wa Yakobo walikuwa watu 70. Wakati huo Yosefu alikuwa amekwisha tangulia kukaa huko Misri.