Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 33:10-24 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Na wawafundishe wazawa wa Yakobo maagizo yako;wawafundishe watu wa Israeli sheria yako.Walawi na wafukize ubani mbele yako,sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni pako.

11. Ee Mwenyezi-Mungu, uzibariki nguvu zao,uzikubali kazi za mikono yao;uzivunjilie mbali nguvu za maadui zao,nguvu za wanaowachukia hata wasiinuke tena.”

12. Juu ya kabila la Benyamini alisema:“Hili ni kabila alipendalo Mwenyezi-Mungu,nalo hukaa salama karibu naye.Yeye hulilinda mchana kutwa,na kukaa kati ya milima yake.”

13. Juu ya kabila la Yosefu alisema:“Mwenyezi-Mungu na aibariki nchi yake,kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,

14. ibarikiwe kwa matunda bora yalioiva kwa jua,kwa matunda ya kila mwezi;

15. kwa mazao bora ya milima ya kale,na mazao tele ya milima ya kale,

16. Nchi yake ijae yote yaliyo mema,ibarikiwe kwa wema wa Mwenyezi-Mungu,ambaye alitokea katika kichaka.Baraka hizi ziwashukie watu wa kabila la Yosefu,aliyekuwa mkuu miongoni mwa ndugu zake.

17. Fahari yake ni fahari ya fahali wa kwanza,pembe zake ni za nyati dume.Atazitumia kuyasukuma mataifa;yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia.Efraimu atakuwa na pembe hizo 10,000na Manase kwa maelfu.”

18. Juu ya kabila la Zebuluni na kabila la Isakari, alisema,“Zebuluni, furahi katika safari zako;nawe Isakari, furahi katika mahema yako.

19. Watawaalika wageni kwenye milima yao,na huko watu watatoa sadaka zinazotakiwa.Maana wao watapata utajiri wao kutoka baharinina hazina zao katika mchanga wa pwani.”

20. Juu ya kabila la Gadi, alisema:“Atukuzwe Mungu ampatiaye Gadi sehemu kubwa.Gadi hunyemelea kama simbaakwanyue mkono na utosi wa kichwa.

21. Alijichagulia eneo zuri kuliko yote,mahali ilipotengwa sehemu ya kiongozi.Aliwaongoza watu na kumtii Mwenyezi-Mungu,alitekeleza mpango wa Mungu kwa Israeli.”

22. Juu ya kabila la Dani alisema hivi:“Dani ni mwanasimbaarukaye kutoka Bashani.”

23. Juu ya kabila la Naftali alisema:“Ee Naftali fadhili,uliyejaa baraka za Mwenyezi-Mungu,nchi yako ni kusini kwenye ziwa Kinerethi.”

24. Juu ya kabila la Asheri alisema:“Asheri abarikiwe kuliko watoto wote wa Yakobo,na upendelewe na ndugu zako wote;na achovye mguu wake katika mafuta.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 33