Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 22:10-20 Biblia Habari Njema (BHN)

10. “Usilime shamba kwa kutumia ng'ombe na punda pamoja.

11. “Usivae mavazi yaliyofumwa kwa sufu na kitani.

12. “Funga vishada katika pembe nne za vazi lako.

13. “Mwanamume akioa mwanamke, halafu baadaye akate shauri kumwacha,

14. na kumshtaki kwamba ametenda mambo ya aibu, na kumharibia sifa kwa kusema kwamba hakupata ushahidi wa ubikira wakati alipomwoa,

15. basi, wazazi wa mwanamke huyo watachukua ushahidi wa ubikira wa binti yao kwa wazee kwenye lango la mji na kuwaambia,

16. ‘Tulimwoza binti yetu kwa mtu huyu, lakini sasa hamtaki tena,

17. na ajabu ni kwamba amemshtaki mambo ya aibu na kusema ati hakumkuta na ushahidi wowote wa ubikira. Hata hivyo ushahidi wa ubikira wa binti yetu ni huu.’ Halafu atakunjua nguo yenye huo ushahidi mbele ya wazee wa mji.

18. Hapo wazee wa mji watamchukua yule mwanamume na kumpiga viboko.

19. Pia watamtoza mtu huyo faini ya vipande 100 vya fedha na kupewa baba wa huyo mwanamke kwa kuwa mwanamume huyo amemharibia sifa binti wa Israeli. Na huyo mwanamke ataendelea kuwa mke wake na hataweza kumpa talaka maisha yake yote.

20. Lakini kama mashtaka hayo ni ya kweli, na hakuna ushahidi wa ubikira wake,

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 22