Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 14:8-18 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Pia msile nguruwe, maana ijapokuwa kwato zake zimegawanyika sehemu mbili, yeye hacheui; hao ni najisi kwenu, msile nyama zao wala msiguse mizoga yao.

9. “Mnaweza kula kila aina ya samaki wenye mapezi na magamba.

10. Lakini kiumbe chochote kinachoishi majini kisicho na mapezi wala magamba msile; hivyo ni najisi kwenu.

11. “Mnaweza kula ndege wote walio safi.

12. Lakini msile ndege wafuatao: Furukombe, kipungu,

13. kengewa, kozi, mwewe kwa aina zake,

14. kunguru kwa aina zake,

15. mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga kwa aina zake,

16. bundi, mumbi, bundi mkubwa,

17. mwari, nderi, mnandi,

18. membe, koikoi kwa aina zake, hudihudi na popo.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 14