Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 14:4-21 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Mnaweza kula wanyama wafuatao: Ng'ombe, kondoo, mbuzi,

5. kulungu, paa, kongoni, mbuzimwitu, paa mweupe, pofu na mbuzi wa mlimani;

6. na kila mnyama mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na mwenye kucheua, huyo mnaweza kula.

7. Lakini msile mnyama yeyote ambaye kwato zake hazikugawanyika sehemu mbili na hacheui; msile ngamia, sungura na pelele, ingawa hucheua lakini kwato zao hazikugawanyika sehemu mbili; hao ni najisi kwenu.

8. Pia msile nguruwe, maana ijapokuwa kwato zake zimegawanyika sehemu mbili, yeye hacheui; hao ni najisi kwenu, msile nyama zao wala msiguse mizoga yao.

9. “Mnaweza kula kila aina ya samaki wenye mapezi na magamba.

10. Lakini kiumbe chochote kinachoishi majini kisicho na mapezi wala magamba msile; hivyo ni najisi kwenu.

11. “Mnaweza kula ndege wote walio safi.

12. Lakini msile ndege wafuatao: Furukombe, kipungu,

13. kengewa, kozi, mwewe kwa aina zake,

14. kunguru kwa aina zake,

15. mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga kwa aina zake,

16. bundi, mumbi, bundi mkubwa,

17. mwari, nderi, mnandi,

18. membe, koikoi kwa aina zake, hudihudi na popo.

19. Na wadudu wote wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.

20. Mnaweza kula viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi.

21. Msile nyamafu yoyote; mnaweza kumpa mgeni anayeishi katika miji yenu, ale, au mnaweza kumwuzia mtu wa taifa lingine, kwa sababu nyinyi ni watakatifu na Mwenyezi-Mungu ni Mungu wenu. Msimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 14