Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 14:12-22 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Lakini msile ndege wafuatao: Furukombe, kipungu,

13. kengewa, kozi, mwewe kwa aina zake,

14. kunguru kwa aina zake,

15. mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga kwa aina zake,

16. bundi, mumbi, bundi mkubwa,

17. mwari, nderi, mnandi,

18. membe, koikoi kwa aina zake, hudihudi na popo.

19. Na wadudu wote wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.

20. Mnaweza kula viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi.

21. Msile nyamafu yoyote; mnaweza kumpa mgeni anayeishi katika miji yenu, ale, au mnaweza kumwuzia mtu wa taifa lingine, kwa sababu nyinyi ni watakatifu na Mwenyezi-Mungu ni Mungu wenu. Msimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.

22. “Toeni sehemu moja ya kumi ya mazao yenu yote ya shambani kila mwaka.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 14