Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 14:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Nyinyi ni watoto wa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu; msijichanje wala kunyoa upara kwa ajili ya mtu aliyefariki.

2. Nyinyi ni watu watakatifu kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu; Mwenyezi-Mungu amewachagua muwe watu wake hasa, kati ya watu wote waishio duniani.

3. “Msile kitu kilicho chukizo kwa Mungu.

4. Mnaweza kula wanyama wafuatao: Ng'ombe, kondoo, mbuzi,

5. kulungu, paa, kongoni, mbuzimwitu, paa mweupe, pofu na mbuzi wa mlimani;

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 14