18. Huwapa haki yatima na wajane; huwapenda wageni na kuwapa chakula na nguo.
19. Basi, wapendeni wageni kwa kuwa nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri.
20. Mcheni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu; mtumikieni; ambataneni naye na kuapa kwa jina lake.
21. Yeye ni fahari yenu; ndiye Mungu wenu ambaye amewatendea haya mambo makubwa na ya kutisha mliyoyaona kwa macho yenu wenyewe.
22. Babu zenu walipokwenda Misri, walikuwa watu sabini tu, lakini sasa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi kama nyota za mbinguni.