Agano la Kale

Agano Jipya

Kumbukumbu La Sheria 10:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Tazama, mbingu hata mbingu za mbingu ni mali yake Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu; dunia na vyote vilivyomo ni mali yake.

15. Tena Mwenyezi-Mungu aliwapenda babu zenu kwa dhati, akawachagua nyinyi wazawa wao kuwa watu wake badala ya watu wengine wote, kama ilivyo hivi leo.

16. Kwa hiyo, takaseni mioyo yenu, msiwe wakaidi tena.

17. Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana. Yeye ni Mungu mkuu na mwenye nguvu, na wa kuogofya; hapendelei wala hapokei rushwa.

18. Huwapa haki yatima na wajane; huwapenda wageni na kuwapa chakula na nguo.

19. Basi, wapendeni wageni kwa kuwa nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri.

20. Mcheni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu; mtumikieni; ambataneni naye na kuapa kwa jina lake.

Kusoma sura kamili Kumbukumbu La Sheria 10